Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Mvulana akiwa ameketi katika moja ya makazi ya wakimbizi wa ndani Goma jimbo la Kivu Kaskazini
© UNICEF/Jospin Benekire

Hali si hali tena DRC mashirika ya UN yataka msaada zaidi na ulinzi kwa raia

Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula duniani WFP leo yametoa wito wa kuchukuliwa hatua mara moja kuwalinda watoto na familia zao waliojikuta katikati ya machafuko yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, huku lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR likielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mustakbali wa zaidi ya raia milioni 7 waliotawanywa na kuomba msaada zaidi kutoka jumuiya ya kimataifa.

Sauti
2'31"
Wapiganaji wa M23 wakielekea Goma DRC, (Kutoka Maktaba)
© MONUSCO/Sylvain Liechti

Nina wasiwasi mkubwa na ukikukwaji wa haki za binadamu katika maeneo yanayokaliwa na M23 – Bintou Keita

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Bintou Keita, ameliambia Baraza la Usalama kwamba ana wasiwasi mkubwa kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa unaofanywa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, ambapo vuguvugu hilo linalenga watendaji wa mashirika ya kiraia, hasa watetezi wa haki za binadamu na waandishi wa habari.

Sauti
2'10"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakishika doria katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. (Maktaba)
MONUSCO/Kevin N. Jordan

DRC: UNHCR yahimiza ulinzi wa raia na upatikanaji wa njia salama za kufikisha misaada

Kufuatia ghasia zilizokithiri wiki iliyopita kati ya vikosi vya serikali na vikundi vya wanamgambo huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo -DRC, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi- UNHCR limeeleza kusikitishwa na athari wanazozipata raia, wakiwemo takriban wakimbizi wa ndani 135,000 walioenda kusaka hifadhi katika mji wa Sake ulio karibu na jimbo la Goma.