Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jean-Marie Guehenno awaarifu waandishi habari juu ya vikosi vya UM kwa Darfur.

Makamu KM juu ya Operesheni za Amani za UM, Jean-Marie Guehenno aliwaarifu waandishi habari wa kimataifa katika Makao Makuu kwamba ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kufanyisha mazungumzo ya hali ya juu na Serekali ya Sudan ili kuondosha hali ya kutofahamiana na kutoaminiana, pindi tumenuia kuwasilisha mafanikio ya kudumu kuhusu pendekezo la kutuma majeshi ya amani ya UM katika Darfur, Sudan.

Mwakilishi wa KM juu ya Usomali ajadilia mchango wa UM nchini.

Mwakilishi wa KM juu ya Usomali, Francois Lonseny Fall wiki hii aliwaarifu waandishi habari wa kimataifa ya kuwa lengo kuu la UM katika Usomali ni kuwahimiza wafuasi wa makundi ya Kiislamu na wawakilishi wa Serekali ya Mpito (TFI) kuendelea kujadiliana na kushauriana juu ya uwezekano wa kurudisha, kipamoja, salama na amani katika taifa lao.~~

Mpango wa Utendaji wa UM Kudhibiti Silaha Ndogo Ndogo Wafanyiwa Mapitio

Miaka mitano baada ya Umoja wa Mataifa (UM) kupitisha Mpango wa Utendaji wa kukabiliana na biashara haramu ya silaha ndogo ndogo na silaha nyepesi katika dunia, Makao Makuu ya UM yalishuhudia mkusanyiko wa hali ya juu wa wawakilishi karibu 2,000 wa kimataifa kutoka serikali wanachama mbalimbali, pamoja na mashirika ya kikanda na kimataifa kwa makusudio ya kuzingatia uwezekano wa kulikomesha tatizo la kuenea kwa silaha ndogo ndogo na silaha nyepesi katika ulimwengu.

Risala ya nasaha ya Katibu Mkuu kwa Umoja wa Afrika(AU).

Katibu Mkuu (KM) wa Umoja wa Mataifa (UM) Kofi Annan kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika (AU)uliofanyika majuzi katika mji mkuu wa Banjul, Gambia aliwaambia wajumbe wa Mataifa Wanachama ya kuwa anajumuika kusherehekea nao, kidhati, mafanikio ya kidemokrasia yaliyojiri miaka ya karibuni katika bara la Afrika.

Mkutano wa UM juu ya Tatizo la Silaha Ndogo Ndogo Duniani.

Mnamo mwaka 2001 wawakilishi wa Mataifa Wanachama katika UM walipitisha, kwa kauli moja, Mpango wa Utendaji uliokusudiwa kuihamasisha jamii ya kimataifa kushirikiana kuratibu kanuni mpya za kuboresha sheria za kitaifa zinazohitajika kudhibiti biashara haramu ya silaha ndogo ndogo ulimwenguni.