Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Haki za Kiutu kutuma ujumbe wa uchunguzi Darfur

Baraza la Haki za Kiutu kutuma ujumbe wa uchunguzi Darfur

Baraza la UM juu ya Haki za Kiutu wiki hii mjini Geneva limepitisha, kwa kauli moja, azimio la kupeleka ujumbe maalumu wa watu watano wa hadhi ya juu, katika jimbo la Darfur, Sudan ili kutathminia na kusailia hali ambayo imeripotiwa kufurutu ada katika utekelezaji wa haki za kimsingi kwa raia.