Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama ya ICTR yataka hukumu ya Seromba irekibishwe

Mahakama ya ICTR yataka hukumu ya Seromba irekibishwe

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) amependekeza hukumu ya kifungo cha miaka 15 aliopewa Athanase Seromba karibuni ibadilishwe kwa sababu anaamini mtuhumiwa huyo aliyekuwa padri wa Parokia ya Nyange, katika kijiji cha Kivumu alishiriki kwenye makosa ya jinai ya hali ya juu iliyohusika na mauaji ya halaiki. Kwa hivyo, Mwendesha Mashitaka angelipendelea Seromba anapewa adhabu kali zaidi.