Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Raia kutoka Mariupol wanakimbia Azovstal eneo la Mariupol kufuatia operesheni ya kuhamishwa inayoongozwa na UN.
© UNOCHA/Kateryna Klochko

Ziara ya Katibu Mkuu wa UN kuhusu Ukraine: “Nafurahia kuripoti mafanikio fulani“

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonip Guterres amelihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo jioni (05-05-2022) na kueleza kuwa wakati wa ziara yake maalum nchini Urusi na Ukriane hakusita kuwaeleza kinaga ubaga bila kupepesa maneno kwa nyakati tofauti na marais wa nchi hizo kwakuwa anataka kuona mzozo na ukatili unaoendelea sasa unamalizika mara moja. 

Wakazi waliosalia Mariupol walikwa wakitumia choo kimoja wakati mji ulikuwa ukiendelea kushambuliwa.
© Alina Beskrovna

Ukraine: Operesheni ya Umoja wa Mataifa na Msalaba Mwekundu inaendelea kuwahamisha raia kutoka kwenye kiwanda kilichoathiriwa cha Mariupol

Operesheni ya Umoja wa Mataifa na Shirika la Msalaba Mwekundu (ICRC) ya kuwaondoa raia waliokata tamaa baada ya kukwama katika kiwanda cha chuma cha Azovstal katika mji wa bandari wa Mariupol nchini Ukraine inaendelea, amethibitisha Msemaji wa ofisi ya masuala ya kibinadamu nchini humo Jumapili.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine
UN /Eskinder Debebe

Guterres awaambia waukraine 'dunia inawaona' huku akiahidi msaada zaidi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameielezea Ukraine kama "kitovu cha maumivu na zahma isiyovumilika", alipozungumza na wanahabari leo mjini Kyiv akiwa pamoja na mwenyeji wake rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na kuahidi kuongeza msaada kwa watu wa taifa hilo huku kukiwa na mateso makubwa , na mamilioni ya watu wamekimbia makazi yao kutokana na uvamizi wa Urusi. 

Mama na mwanae wakiondoka kituo cha treni cha Lvivi nchini Ukraine.
© UNICEF/Giovanni Diffidenti

Mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani Ukraine:IOM

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM inasema mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani nchini  Ukraine na hivyo kuifanya idadi ya watu waliokimbia makazi yao na kusalia wakimbizi wa ndani tangu kuanza kwa mzozo wa Ukraine tarehe 24 mwezi Februari mwaka huu kufikia zaidi ya watu milioni 7.7 sawa na asilimia 17 ya watu wote wa taifa hilo.

Sauti
1'59"