UNICEF imetanabaisha kuhusu hatari kubwa za afya ya akili kwa watoto wa Ukraine
Wiki kumi baada ya vita kuzuka nchini Ukraine, wasaidizi wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamesema kwamba wanaongeza haraka juhudi za kuwapa watoto walio katika mazingira magumu msaada wa kitaalamu na kisaikolojia, huku kukiwa na mahitaji mkubwa ya afya ya akili na hatari zinazoendelea zinazohusiana na uvamizi wa Urusi na ukatili wa kingono na kijinsia.