Siku 100 za uvamizi wa Urusi kwa Ukraine, ustawi wa watu umeathirika sana
Leo ni siku 100 tangu kuanza kwa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ulioanza tarehe 24 Februari mwaka huu. Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wake wanasema katika hizi siku 100 tu, uvamizi huu ambao ni ukiukaji wa Katiba ya Umoja wa Mataifa, umewaweka watu wa Ukraine katika hali ya kutisha.