Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres akizungumza na wanahabari jijini New York, Marekani mbele ya bunduki iliyokunjwa inayoashiria usalama au bila mapigano.
UN /Eskinder Debebe

Pasaka ya waothodoksi Ukraine na Urusi ikikaribia, sitisheni mapigano kwa siku 4: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa siku nne za sitisho la mashambulizi nchini Ukraine kuanzia Alhamisi ya wikii hii wakati huu ambapo wiki takatifu ya kuelekea sikukuu ya PAsaka kwa waumini wa madhehebu ya kikristo ya kiothodoksi nchini Ukraine ikianza keshokutwa Alhamisi. Ametaka sitisho hilo liendelee hadi Jumapili tarehe 24 mwezi huu kilele cha Pasaka ya kiothodoksi.