Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Raia wa Panama wenye asili ya Afrika wanatumia sauti zao kutokomeza ubaguzi wa rangi na ubaguzi.
UN Panama/Javier Conte

Ubaguzi rangi watia sumu kwenye taasisi na jamii - Guterres

Ubaguzi umeendelea kutia sumu kwenye taasisi, miundo ya kijamii na katika maisha ya kila siku, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo wakati wa mkutano maalum wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofanyika jijini New York, Marekani juu ya kile kinachoitwa kuwa kichocheo cha kuhalalisha chuki, kupinga utu na kusambaza ghasia.

 

Bibi akmhudumia mjukuu wake kwenye hospitali ya watoto mjini Kyiv nchini Ukraine
© UNICEF/Oleksander Ratushniak

Vita Ukraine yasababisha uhaba wa Oksijeni itumikayo kutibu wagonjwa - WHO

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo tena limekutana kujadili vitisho vya amani na usalama duniani ikijikita zaidi katika uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ambapo Mkuu wa Idara ya siasa kwenye Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo amesema dalili nzuri zilizoonekana wiki hii kufuatia mazungumzo kati ya wawakilishi wa mataifa hayo mawili bado hazijazaa matunda yoyote.