UNHCR yalani ubaguzi kwa baadhi ya watu wanaokimbia Ukraine
Kamishna mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, leo amezungumza dhidi ya hali mbaya kuhusu baadhi ya wakimbizi wanaokimbia kuvuka mpaka wa Ukraine, na raia wa nchi ya tatu, kwamba wamekuwa wakikabiliwa na ubaguzi wa rangi na ubaguzi mwingine.