Mahakama ya ICC yatoa waranti ya kukamatwa kwa Rais Putin wa Urusi
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu inayoungwa mkono na Umoja wa Msataifa ICC leo imetoa hati au waranti ya kukamatwa kwa Rais Vladimir Putin wa Urusi kuhusiana na madai ya uhalifu wa kivita kuhusu kurejeshwa kwa lazima na uhamishaji haramu wa watoto kutoka eneo linalokaliwa la Ukraine amesema mkuu wa ICC.