Ukraine-Urusi: Baraza la Usalama lakutana kwa dharura
Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kimefanyika alasiri ya Jumamosi tarehe 31 baada ya kuitishwa na Urusi kufuatia mashambulizi huko Belgorod mpakani na Ukraine, mashambulizi ambayo Afisa Mwandamizi wa Umoja wa Mataifa amelaani.