Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Familia kutoka Eritrea ikiwa kwenye kituo cha muda Romani wakisubiriwa kuhamishwa hadi Netherlands.
© UNHCR/Stefan Lorint

Idadi ya wasaka hifadhi nchi ya tatu kuongezeka 2023

Zaidi ya wakimbizi milioni 2 mwaka ujao WA 2023 watahitaji kuhamishiwa nchi ya tatu ikiwa ni ongezeko kwa asilimia 36 ikilinganishwa na mahitaji ya mwaka huu ambayo ni wakimbizi milioni 1.5 pekee, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia tathmini ya makadirio ya kuhamia nchi ya tatu kwa mwaka 2022.

Mji wa Bucha umeharibiwa vibaya kufuatia mashambulio Kyiv, mji mkuu wa Ukraine.
© WFP/Marco Frattini

Taarifa za awali zadokeza uhalifu wa kivita na ukiukwaji wa haki za binadamu Ukraine- Kamisheni 

Kamisheni iliyoundwa na Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu kuchunguza madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kibinadamu nchini Ukraine imetoa ripoti ya ziara yake ya kwanza nchini Ukraine na kusema ingawa haiko katika nafasi ya kuwa na vigezo vya kisheria au matokeo kamilifu, taarifa za awali zinadokeza kuweko kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kiutu. 

Mji wa bandari wa Mariupol ulioshambuliwa nchini Ukraine.
IOM/Diana Novikova

Vita Ukraine: Bei za nishati, chakula zazidi kupaa 

Zaidi ya siku 100 zimepita tangu Urusi kuvamia Ukraine, na hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametambulisha ripoti ya pili kutoka kikundi cha kuchukua hatua dhidi ya janga la dunia litokanalo la vita hivyo, GCRG na kusema madhara ya vita hiyo katika sekta ya chakula, nishati na fedha ni dhahiri shairi na yanazidi kuongezeka kila uchao.

Mvulana akitembelea karibu na majumba yaliyosambaratishwa jirani na nyumbani yao huko Novoselivka, viunga vya mji wa Chernihiv nchini Ukraine
© UNICEF/Ashley Gilbertson

Mambo 5 ya kufahamu kuhusu kulinda raia dhidi ya silaha za mlipuko vitani

Kwa wastani, asilimia 90 ya wanaouawa na kujeruhiwa kwa silaha za milipuko zinazotumiwa katika maeneo yenye wakazi wengi ni raia.  Ahadi ya kisiasa ya kukabiliana na madhara ya kibinadamu yanayoongezeka kutokana na matumizi ya silaha hizo katika miji mikubwa, miji midogo na vijijini inaweza kuwa hatua kubwa kuelekea kuwalinda wale walioko kwenye maeneo ya migogoro na vita.