Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukraine

UNDP inasaidia kutegua mabomu ya ardhini nchini Ukraine.
UNDP in Ukraine/Alexander Ratushnyak

Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa: Paul Heslop

Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. 

Sauti
2'33"
Olga (kushoto) akiwa na mbwa na mtoto wake, waathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine.
UNHCR Video

Bila UNHCR sijui ningekaa wapi: Olga muathirika wa vita Ukraine

Kutana na Olga mwathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine ambaye baada ya nyumba yake kushambuliwa na kombora mjini Borodyanka alikataa tamaa ya Maisha lakini sasa mradi wa UNHCR wa kukarabati nyumba zilizoharibiwa na vita Ukraine umemfufulia matumaini ya Maisha yeye na mwanaye “Katika maisha mambo hayawezi kuwa mteremko tu, kuna wakati unapitia magumu na ukiwa na uvumilivu utayashinda.

Sauti
3'9"
Jengo lililoharibiwa katikati mwa Kharkiv, Ukraine.
© UNOCHA/Matteo Minasi

Viongozi watoa maoni yao baada ya uamuzi wa Baraza Kuu la UN dhidi ya Urusi

Vita ya Ukraine ikiwa inaingia mwaka wake wa pili, wawakilishi mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametoa maoni yao kufuatia uamuzi kwa njia ya kura uliofanywa na Kikao Maalumu cha  dharura cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio jipya la kutaka amani ya haki na ya kudumu nchini Ukraine na kwamba Urusi bila masharti yoyote iondoe mara moja majeshi yake katika ardhi ya Ukraine. 

Sauti
2'22"
Leo ni Siku ya uhuru wa Ukraine hapa ni mjini Kyiv
© UNDP Ukraine/Krepkih Andrey

Miezi sita ya vita nchini Ukraine haya ni baadhi ya yaliyofanywa na WFP

Hii leo imetimia miezi sita rasmi tangu kuanza kwa vita baina ya Ukraine na Urusi baada ya Urusi kuivamilia Ukraine vita ambayo si tu imeleta madhara na maafa kwa Ukraine bali dunia kwa ujumla ikiwemo kupandisha bei za mafuta na chakula. Katika siku hiii tuangalia machache yaliyofanywa na moja tu la mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa lile la Mpango wa Chakula duniani WFP katika kuwasaidia wananchi wa Ukraine.

Sauti
3'5"