UNMISS yalaani shambulio katika kaunti ya Mayom nchini Sudan Kusini
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, umelaani shambulizi lililotokea Julai 22 mwaka huu 2022 katika Kaunti ya Mayom, iliyoko katika jimbo la Umoja nchini humo na kusababisha vifo vya watu kadhaa akiwemo Kamishna wa Kaunti hiyo ya Mayom.