Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Kambini Kakuma
UN/Esperanza Tabisha

Wakimbizi tukikirimiwa tunarejesha fadhila kwa jamii:Bahati, Micheline na Agnes

Kutana na wakimbizi Bahati Hategekimana kutoka Rwanda, Micheline Muhima kutoka Uganda na Agnes Mude kutoka Sudan Kusini ambao wote walikuwa wakiishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, lakini sasa kupitia mradi wa majaribio wa kuthamini mchango wa wakimbizi EMPP, unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mjini Pictou na serikali ya Canada watatu hao si wakimbizi tena bali ni wafanyakazi wa huduma ya jamii kwenye kituo cha Glen Haven Manor kilichopo jimboni Nova Scotia nchini Canada. 

Sauti
2'34"
Mfanyakazi wa UNMAS akichunguza mabomu ya kutegwa ardhini, jimbo la Equatoria kati, Sudan Kusini.
© UN Photo/Isaac Billy

UNMAS yaendelea kunusuru maisha ya watu Sudan Kusini kwa kutegua mabomu ya kutegwa ardhini 

Wakati hatua kubwa imepigwa katika kuondoa na kutegua mabomu yote ya kutegwa ardhini na mabaki mengine ya vifaa vya milipuko ya vita nchini Sudan Kusini, baadhi ya jamii za nchi hiyo bado ziko hatarini kutokana na uwepo wa mabomu hayo. Moja ya jamii hizo ni  Gondokoro karibu na mji mkuu Juba, ambako kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya huduma za kutegua mabomu ya kutegwa ardhini UNMAS kazi kubwa inaendelea kuyaondoa kabisa mabomu hayo.

Sauti
2'58"
Mapigano ya kikabila katika eneo la Jonglei nchini Sudan Kusini yamesababisha utekaji nyara na mauaji. (Maktaba))
UNMISS

Mzozo wa wakulima na wafugaji Sudan Kusini wasababisha vifo vya zaidi ya watu 130 

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS umechukua jukumu la kuwaleta pamoja raia na vyombo vya usalama vya serikali ili kuzungumza na kusaka amani kufuatia migogoro baina ya wakulima wakazi wa Magwi na wafugaji wanaohamahama, mapigano ambayo yamesababisha vifo vya watu 130 pamoja na kuchochea vitendo vya udhalilishaji.

Sauti
2'38"