Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Mafuriko ya hivi karibuni nchini Sudan Kusini
Picha: UN News

Msaada wa dola milioni 14 kutoka CERF kunufaisha zaidi ya watu 260,000 Sudan Kusini

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya dharura, Martin Griffiths ametangaza kutoa dola million 14 kutoka mfuko mkuu wa dharura wa Umoja huo, CERF kwa ajili ya kupatia misaada ya kibinadamu wananchi wa Sudan Kusini walioathiriwa na ongezeko la mapigano na mafuriko, kwa kuzingatia kuwa ombi la usaidizi kwa taifa hilo bado uchangiaji wake unasuasua. 

Mama amempeleka mwanye aliyeathirika vibaya na utapiamlo kwenye kituo cha lishe cha WFP Torit nchini Sudan Kusini
© WFP/Eulalia Berlanga

Mabadiliko ya tabianchi yazidisha zahma ya utapiamlo na njaa Sudan Kusini:UNICEF/FAO/WFP 

Umoja wa Mataifa umeonya hii leo kuwa njaa na utapiamlo vinaongezeka katika maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko, ukame na mizozo nchini Sudan Kusini huku baadhi ya jamii zikiwa hatarini kukumbwa na njaa iwapo misaada ya kibinadamu haitakuwa endelevu, halikadhalika mikakati ya kukabili madhara ya mabadiliko ya tabianchi haitaimarishwa. 

Michael Dunford, Mkurugenzi wa WFP Pembe ya Afrika akihojiwa na UN News.
UN/ Leah Mushi

Hatari ya baa la njaa bado ni jinamizi linaloizonga Somalia: WFP Dunford

Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa Kenya, Ethiopia na Somalia nchi ambayo maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako mstari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.

Sauti
2'
Soko nchini Sudan Kusini
© UNICEF/Sebastian Rich

UNMISS yapatia mafunzo wafanyabiashara Sudan Kusini ili wafanye biashara kwa ufanisi

Ushirikiano na ukuaji kiuchumi ni miongoni mwa masuala muhimu katika kuhakikisha nchi yoyote ina amani na wananchi wake wanapata Maendeleo. Na ili kuhakikisha wananchi wa Sudan Kusini wana amani na maendeleo, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda Amani nchini humo UNMISS umeandaa warsha ya biashara lengo likiwa ni kuwatia moyo wafanyabiashara wa ndani na kuwawezesha kiuchumi ili nao waweze kuimarisha biashara zao lakini pia waweze kufanya biashara na Umoja wa Mataifa .

Sauti
3'34"
Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

Makamu wa Rais wa Sudan Kusini Hussein Abdelbagi Akol Agany akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu UNGA77
UN Photo/Cia Pak

Amani inaimarika Sudan Kusini lakini bado tuna changamoto: Agany

Amani nchini Sudan Kusini inaendelea kuimarika huku idadi kubwa ya wakimbizi wa ndani wameanza kurejea katika makazi yao kwenye maeneo ambako utulivu umerejea na serikali inafanya kila iwezalo kuhakikisha mkataba wa amani unadumiswa amesema makamu wa Rais wa Sudan Kusini Hussein Abdelbagi Akol Agany akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza kuu hii leo mjini New York Marekani.

Sidonie, mwenye umri wa miaka 10, akiwa mbele ya darasa la shule yake ya msingi Kitambo iliyoko mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Kinshasa.
© UNICEF/Josue Mulala

Elimu ya sasa inapitia janga kubwa: Tuirekebishe kwa mustakabali wa watoto

Ingawa msemo wa haki ya binadamu umezoelekea, hakuna haki ya binadamu yoyote ambayo imetolewa bure bila kupiganiwa, vivyo hivyo inapaswa kuwa kwa elimu, amesema Leonardo Garnier, Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani, mkutano unaoanza Ijumaa hii kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Kufahamu msingi wa kauli hiyo, 

Sauti
2'