Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Katika picha hii kutoka maktaba, Ronda, (kulia) mmoja wa wakimbizi wa ndani akifua nguo zake kwenye kituo cha kufadhi raia huko Wau Sudan Kusini.
UNICEF/Ohanesian (maktaba)

Kiu ya amani Sudan Kusini ni dhahiri- Shearer

Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan kusini, David Shearer, ametembelea eneo la Bahr El Ghazal nchini humo ambako amekuwa na mazungumzo na viongozi kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa mkataba wa amani, kusaidia wakimbizi wa ndani kurejea kwa hiyari katika maeneo yao na pia kuhusu suala la usalama katika ukanda huo.

Sauti
1'43"
Mwanamke akichora kwenye ukuta maandishi yanayosema amani, katika mji wa yei
UNMISS/Denis Louro

UNMISS yatathimini hali ya Yei Sudan Kusini

Wakati jitihada za kutekeleza makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mnamo mwezi Septemba mwaka 2018 zikiendelea mjini Yei Sudan Kusini, eneo la kilimo ambalo liliwahi kuwa chanzo kikuu cha chakula nchini humo bado linakabiliana na ukikukwaji mkubwa wa haki za binadamu na watu kuyahama makazi yao. 

Sauti
2'39"