Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Mlinda amani wa UNMISS akishika doria katika barabra karibu na Bentiu, jimbo la Unity, Sudan Kusini.
UNMISS Photo

Vikosi vya Umoja wa Mataifa Sudan Kusini vinawapeleka wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.

Walinda amani Sudan Kusini wasindikiza wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.Polisi waliopo kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini  wamepewa jukumu la kuwasindikiza wanafunzi hadi kwenye kituo cha mtihani kwenye mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.  Usindikizaji huo unafanyika Kwa wiki mbili ambapo askari hao wataendelea kuwapeleka na kuwarudisha wanafunzi kufanya mitihani yao kwa usalama.

Sauti
1'57"
Kutoka kushoto: Bendera ya UN ikipepea New York; Naibu Katibu Mkuu akiwa na nakala ya ripoti ya  UNCTAD; Walinda amani wa UN; Katibu Mkuu akiwa na wanawake viongozi waandamizi wa UN
UN

Zilizovuma mwaka 2018

Mwaka 2018 ulighubikwa na changamoto nyingi hususan kwa nchi za Afrika, mizozo ikiendelea kukumba bara hilo sambamba na magonjwa. Hata hivyo kulikuwa na habari chanya, na kwa muhtasari tutaangazia pande zote za sarafu wakati huu ambapo tunafunga mwaka huu wa 2018.