Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Matatizo ya muda mrefu yamesababisha mateso makubwa kwa watu wa Sudan Kusini hasa  wanawake.
UN Photo/Isaac Billy

Maafisa wenye mamlaka wamehusika na ukiukwaji wa haki Sudan Kusini - Ripoti

Ripoti ya tume ya  Haki za Binadamu nchini Sudan Kusini  iliyowasilishwa leo mijini Geneva Uswisi, imebaini kuwa watu 23 katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita waliokuwa katika ngazi ya mamlaka nchini humo, wanakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji  mkubwa wa haki za binadamu chini ya sheria za kimataifa kwa kutekeleza uhalifu mkubwa unaohusiana na vita nchini Sudan kusini.

Michelle Bachelet, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa akihutubia Machi 6, 2019 Kikao cha Baraza la Haki kuhusu hali ya haki za binadamu duniani.
UN /Violaine Martin

Japo pengo la usawa linaweza kusambaratisha mihilili ya UN, haki inaleta matumaini:Bachelet

Ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaendelea kutamalaki katika sehemu mbalimbali duniani ukichochewa zaidi na changamoto zilizopo hivi sasa ikiwemo tishio la mabadiliko ya tabianchi, maendeleo ya teknolojia, vita vinavyozua zahma kubwa kwa raia, ukosefu wa ajira kwa vijana, mabadiliko ya mifumo, chuki dhidi ya wageni na ongezeko la pengo la usawa.

Kituo cha Umoja wa Mataifa cha kulinda Raia, Wau, Sudan Kusini.
UN

Mahakama ya kuhamahama yapeleka haki Malakal, Sudan Kusini.

Kwa zaidi ya kipindi cha siku tatu, mahakama ya kuhamahama inayofadhiliwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS, imekuwa katika mji wa Malakal  jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini ili kushughulikia kesi kadhaa zikiwahusisha watu ambao walitenda makossa makubwa yakiwemo kesi mbili za unyanyasaji wa kingono na moja ya unyanganyi kwa kutumia silaha.

Sauti
2'28"
Mwanamke mkazi wa Wau Shilluk Sudan Kusini, mji ambao umeharibiwa na mapigano yaliyosambaratisha makazi, shule na hospitali.
UNICEF/UN0236862/Rich

Vita na ukwepaji sheria lazima vikome Sudan Kusini:UN ripoti

Wakati maelfu ya watu kwa mara nyingine wakifurushwa makwao kwa sababu ya machafuko nchini Sudan kusini , tume ya haki za binadamu kwa ajili ya Sudan Kusini imeitaka serikali ya nchi hiyo na pande zote katika mzozo kuheshimu mkataba wa usitishaji uhasama na kutekeleza mkataba huo mpaya wa amani uliotiwa saini miezi mitano iliyopita.

Sauti
2'25"