Kikosi cha 8 cha Tanzania cha kulinda amani, TANZBATT-8 chawasili DRC na mipango madhubuti.
Kikosi cha 8 cha Tanzania, TANZBATT-8 kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO.
Kikosi cha 8 cha Tanzania, TANZBATT-8 kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO.
Kufuatia serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutangaza kifo cha mtu mmoja huko Butembo jimboni Kivu Kaskazini kutokana na ugonjwa wa Ebola, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limepeleka wafanyakazi zaidi na linajiandaa kupeleka vifaa vya matibabu.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR, inasikitishwa na ongezeko kubwa la matukio ya mashambulizi ya raia kwenye maenoe ya Irumu na Mambasa jimboni Ituri halikadhalika eneo la Beni katika jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Noela Kombe al maaruf Mamaa Noela ni mwanamke shujaa aliyejizolea umaarufu mkubwa kwa kujitolea kulea watoto yatima na waishio katika mazingira magumu licha ya kuwa na changamoto nyingi anazo kumbana nazo wakati wa uendeshaji wa kituo hicho cha Mungu ni Mwema kilichopo eneo la Beni mjini jimboni Kivu kaskazini nchini jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC.
Hatimaye matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na Umoja wa Mataifa kwa wakazi wa dunia kuhusu udharura wa janga la tabianchi yametolewa hii leo huku asilimia 64 ya washiriki wakitambua umuhimu wa hatua za dharura dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na hivyo kuwepo kwa hatua mahsusi za makusudi ili kukabili janga la tabianchi linalokumba dunia hivi sasa.
Nchini Zambia shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limechukua hatua kusaidia jimbo la Luapula lililoko mpakani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kuwa na huduma za kujisafi na maji safi, WASH kwa lengo la kuondokana na magonjwa ya kuambukiza na pia kupatia watoto fursa ya kutosha ya kujifunza.
Walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu katika kikundi cha TANZBATT-7 ambacho kiko katika kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB, cha Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO, wametembelea na kutoa zawadi kwa watoto wa kituo cha Mungu ni mwema, Beni, DRC.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wamechukua jukumu la kufundisha wakazi wa jimboni Kivu Kaskazini teknolojia ya mawasiliano kama njia mojawapo ya kuwajengea uwezo sambamba na ulinzi wa raia.
Bintou Keita wa Guinea ameteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kuwa mwakilishi wake maalum nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejea wito wake wa kusitisha uhasama kimataifa na kuyataka makundi yote yenye silaha kuweka silaha hizo chini na kujiunga katika mchakato wa amani, baada ya raia zaidi ya 20 kuuawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.