Kikosi cha 8 cha Tanzania cha kulinda amani, TANZBATT-8 chawasili DRC na mipango madhubuti.
Kikosi cha 8 cha Tanzania cha kulinda amani, TANZBATT-8 chawasili DRC na mipango madhubuti.
Amani na Usalama
Kikosi cha 8 cha Tanzania, TANZBATT-8 kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO.
Kwa mujibu wa makamanda wa ngazi za juu wa Jeshi la Tanzania, kikosi hiki pamoja na vikosi vingine, vitakuwa na uwezo wa kuchukua hatua za haraka zaidi kukabiliana na vitisho na hatimaye kuimarisha ulinzi wa raia nchini humo. Zaidi kuhusu kuwasili kwa TANZBATT-8, na mipango yao katika kipindi chote watakachukuwa nchini DRC, Afisa Habari wa kikosi hicho kipya, Kapteni Tumaini Bigambo ametutumia taarifa ifuatayo.