Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Walinda amani wa TANZBATT-7 watoa zawadi kwa watoto yatima DRC.

Eneo la Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC, Cecile ambaye ni yatima akitoa shukrani baada ya kituo chao cha yatima, Mungu ni Mwema kupokea msaada kutoka kwa walinda amani wa Tanzania, TANZBATT_7
TANZBATT_7/ Issa Mayambua
Eneo la Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC, Cecile ambaye ni yatima akitoa shukrani baada ya kituo chao cha yatima, Mungu ni Mwema kupokea msaada kutoka kwa walinda amani wa Tanzania, TANZBATT_7

Walinda amani wa TANZBATT-7 watoa zawadi kwa watoto yatima DRC.

Amani na Usalama

Walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu katika kikundi cha  TANZBATT-7 ambacho  kiko katika kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB, cha Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO, wametembelea na kutoa zawadi kwa watoto wa kituo cha Mungu ni mwema, Beni, DRC. 

 

 

Msaada huo wa vyakula na mahitaji mengine ya kibinadamu umepokelewa kwa furaha na watoto ambao wanalelewa katika kituo cha Mungu ni mwema.  Mwanahabari Luteni Issa Mwakalambo, Afisa habari wa TANZBATT-7 ameshuhudia tukio hilo na anaeleza zaidi.