Harakati za Tanzania na wadau za kurekebisha mfumo wa elimu
Mazungumzo ya kimkakati ya ngazi ya juu kati ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania na wadau wa maendeleo yalifanyika nchini humo tarehe 24 mwezi Novemba mwaka jana wa 2023 yakiangazia mwelekeo wa marekebisho ya mfumo wa elimu katika taifa hilo la Afrika Mashariki.