Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Kitongoji hiki huko Bucha kiliteseka sana wakati wa uvamizi wa Urusi. Nyumba hii ilipigwa bomu. Leo kila kitu kimerejeshwa kabisa.
UN News/Anna Radomska

Ukraine: Bucha na Irpin zinaibuka kutoka kwenye majivu ya uvamizi wa jeshi la Urusi

Wakati uvamizi wa Urusi huko Bucha katika siku za mwanzo za uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, ulimalizika mnamo Machi 2022, uharibifu mkubwa ulionekana, na tume ya Umoja wa Mataifa ikihitimisha kwamba uhalifu wa kivita ulikuwa umetendwa dhidi ya raia, miaka miwili baadaye, maisha yanarudi katika mji ulio nje kidogo ya Kyiv, ambao umerejeshwa kwa msaada wa UN.

Julian Assange akizungumza na vyombo vya habari mjini London Uingereza (Kutoka Maktaba)
© Foreign Ministry of Ecuador/David G. Silvers

MAHOJIANO: Mtaalamu huru wa UN anaonya juu ya athari za kumuhamishia Assange Marekani

Kabla ya kusikilizwa kwa kesi iliyopangwa ya Julian Assange nchini Uingereza, ambako kuna uwezekano mkubwa atarejeshwa Marekani kwa lazima, mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kuhusu uwezekano wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya mwanzilishi huyo wa WikiLeaks, akionya zaidi kwamba kuanathari za kesi hiyo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa uandishi wa habari duniani na uhuru wa kujieleza.

Kipepeo aina ya monarch hukusanya nekta kutoka kwenye mmea wa mbigili (thistle plant).
Unsplash/Sean Stratton

Bioanuwai: Ni nini, na tunawezaje kuilinda?

Umoja wa Mataifa na wadau wake ulimwenguni wanakabiliana na upotevu mkubwa wa wanyama na mimea, tarehe 23 Januari wanakutana jijini Nairobi, kenya kujadili jinsi ya kuepuka upotevu huo, katika mkutano mkuu ambao utaangazia bioanuwai ni nini, na jinsi gani Umoja wa Mataifa, unaweza kusaidia juhudi za kuwezesha asili kuishi na kustawi.