Ukraine: Bucha na Irpin zinaibuka kutoka kwenye majivu ya uvamizi wa jeshi la Urusi
Wakati uvamizi wa Urusi huko Bucha katika siku za mwanzo za uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, ulimalizika mnamo Machi 2022, uharibifu mkubwa ulionekana, na tume ya Umoja wa Mataifa ikihitimisha kwamba uhalifu wa kivita ulikuwa umetendwa dhidi ya raia, miaka miwili baadaye, maisha yanarudi katika mji ulio nje kidogo ya Kyiv, ambao umerejeshwa kwa msaada wa UN.