Jifunze Kiswahili: Uchambuzi wa neno, "RUWI"
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunafafanuliwa maana ya neno "RUWI" na mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, Karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunafafanuliwa maana ya neno "RUWI" na mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, Karibu!
Ubunifu ni moja ya mambo yanayotazamwa kuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Nchini Uganda, msichana Jovia Kyomuhendo amepata sifa kwa kuwa kijana mbunifu ambaye amefikia hatua ya kujiajiri kwa kuanzisha kiwanda kidogo cha kushona na pia kutengeneza viatu.
Safari yake imekuwaje hadi kufikia kutunukiwa tuzo na Muungano wa Viwanda Vidovidogo nchini Uganda USSIA? Tupate taarifa zaidi kutoka kwa mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego.
Janga la corona au COVID-19 limeendelea kuitikisa dunia kijamii na kiuchumi karibu kila pembe ya ulimwengu. Na hali ndivyo ilivyo kwa wavuvi wa ziwa Tanganyika mkoani Kigoma ambako Devotha Songorwa kutoka Radio washirika TanzaniakidsTime FM amezungumza na wavuvi mbalimbali wa ziwa Tanganyika mkoani huo kutaka kujua je wanafahamu nini kuhusu janga hili , limewathiri vipi, na endapo wanatambua kuhusu suala la chanjo na umuhimu wake katika kuwanusuru wavuvi na sekta hiyo wakati huu wa janga la COVID-19? Ungana nao katika Makala hii.
Kila siku wananchi watano katika kijiji cha Pazhaki jimboni Kabul nchini Afghanisan walikuwa wanajukumu la kufungulia maji katika mfereji uliokuwa unategemewa na wanakijiji hao kwa shughuli za kilimo. Lakini Ramazan Ibrahimkil, mwenyekiti wa Kijiji cha Pazhak anasema alikuwa anapokea kesi kila uchwao kwamba wananchi wanaokaa milimani wakilalamikiwa kufungulia maji kwa wingi na hivyo wale wa mabondeni kukosa maji ya kutosha kwenye kilimo chao na hivyo kupata mazao machache na kipato kidogo.
Kikao hiki cha 65 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani kilichoanza tarehe 15 Machi kikiwa sasa kinakamilisha wiki yake ya kwanza, wadau kwa namna mbalimbali kote duniani wanaendelea kujadili mada ya mwaka huu ambayo imejikita kwenye kuangazia wanawake katika uongozi ili kufikia dunia yenye usawa.
Katika makala ya wiki hii tunamulika hatua zinazochukuliwa na Umoja wa Mataifa na wadau wake kutekeleza tamko la haki za binadamu la mwaka 1948 ambalo mwaka huu limetimiza miaka 72.
Kuelekea siku ya udongo duniani tunaangazia mradi wa Shirika la chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kupitia mradi wa pamoja wa Kigoma (KJP) wa mafunzo kwa wakazi wa Kigoma nchini Tanzania.
Kwa upande wake Elizabeth Mrema Katibu mtendaji wa sekretarieti ya mkataba wa kimataifa kuhusu masuala ya Bayonuai (CBD) anasisitiza umuhimu wa kutunza bayonuai ya udongo.
Leo tunamulika ni kwa jinsi gani uwepo wa kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO umekuwa ni nuru kwa vijana na wafanyabiashara wa eneo la jimbo la Kivu Kaskazini. Shuhuda wetu huko si mwingine bali Luteni Issa Mwakalambo, afisa habai wa kikosi cha Saba cha Tanzania,
Leo ni siku ya watoto duniani ikimulika kile ambacho kila mtu anafanya kuhakikisha kuwa dunia ni salama kwa mtoto wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19. Umoja wa Mataifa una hofu kuwa janga hili linaweza kutowesha uzingatiaji wa misingi mikuu minne ya haki za mtoto ambayo ni kuishi, kuendelezwa, kushirikishwa na kulindwa. Je nini kinafanyika mashinani? Watoto wenyewe wanasemaje? Basi tumulike hali Afrika Mashariki.
Tukielekea siku ya kisukari duniani hapo kesho shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linasema idadi ya wagonjwa wa kisukari duniani inaongezeka na ugonjwa huo unakatili maisha ya watu…. Kila mwaka. Ndio maana mwaka huu kaulimbiu ni waauguzi na kisukari ikiwa ni kampeni ya kuelimisha kuhusu umuhimu wa jukumu la watu hao katika vita dhidi ya kisukari. Hata hivyo unapokuwa mkimbizi katika mkambini au makazi ya wakimbizi ukitegemea msaada kuweza kuishi kisukari ni msumari wa moto juu ya kidonda.