Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

UN News

Kiswahili kuanza kutumika EAC rasmi mwaka 2024

Lengo namba 17 la Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs linataka uwepo wa Ushirikiano katika kufanikisha malengo. Ushirikiano huo unaweza kuwa baina ya nchi na nchi, wananchi na ushirikiano wa kikanda. Mwezi Desemba mwaka jana 2023 nilifunga safari hadi jijini Arusha nchini Tanzania na kuzungumza na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Peter Mathuki kutaka kufahamu namna wanavyoshirikiana na Umoja wa Mataifa katika maeneo mbalimbali ikiwemo ulinzi na usalama pamoja na kukuza lugha ya Kiswahili. Karibu usikilize mazungumzo yetu. 

Sauti
7'40"

28 DESEMBA 2023

Hujambo na karibu kusikiliza jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili  ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni Alhamisi ya tarehe 28  ya  mwezi Desemba takribani siku 4 panapo majaliwa kuumaliza mwaka huu wa 2023. Mimi ni ASSUMPTA MASSOI ninakukaribisha kusikiliza mkusanyiko wa matukio machache kati ya mengi yaliyojiri katika mwaka huu ambapo Umoja wa Mataifa ulikuwa na jukumu zito kuhakikisha pamoja na yote bado dunia inasalia kuwa mahali salama pa kuishi. 

Sauti
14'9"
Habari za UN

Jifunze Kiswahili - "KUMBITI"

Katika jifunze Kiswahili hii leo tunabisha hodi kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA  Je wajua maana ya neno “KUMBITI”? 

Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA anafafanua. 

Sauti
47"

20 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea maoni kuhusu matumizi ya lugha ya kiswahili kutokwa kwa viongozi wanaoshiriki UNGA78, na yaliyojiri hapa makao makuu katika mjadala kuhusu malengo ya maendeleo endelevu. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani tunasalia hapa makao makuu, kulikoni?  

Sauti
14'56"
UN/ Stella Vuzo

Tuzungumze Kiswahili kwenye UNGA78 - Viongozi wa EAC

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Peter Mathuki amesema ili kuongeza ushawishi na kukuza lugha ya Kiswahili duniani ni vyema viongozi wa jumuiya wakazungumza lugha hiyo wakiwa katika mikutano mikubwa duniani akitolea mfano mjadala Mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA78.  

Sauti
3'36"
Habari za UN

Methali: "Ukubwa jalala"

Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia methali isemayo “Ukubwa ni jalala.”

Sauti
1'39"

11 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo ninatupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kama ilivyo sehemu nyingi za Afrika Mashariki nako lugha ya kiswahili inatajwa kuwa chombo chenye nguvu sana kinachoingilia kati ujenzi wa amani na pia katika biashara hasa kwa wakaazi wa mji wa Goma katika jimbo la Kivu Kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Kiswahili ndio lugha ya kwanza nchini DRC yenye idadi kuwa ya wazungumzaji katika mikoa ya Mashariki na Magharibi mwa nchi ambako inatumiwa hata kwenye vyombo vya habari kama Redio na televisheni.

Sauti
10'50"