Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

04 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani kubwa ni mada kwa kina ikitupeleka nchini Kenya ambako mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa Thelmwa Mwadzaya ametembelea shule inayosomesha watoto wa kike bila malipo, watoto ambao wako hatarini kukumbwa na ndoa za utotoni na ukeketaji au FGM. Nini kinfanyika? Na wazazi wanasemaje? 

Sauti
12'24"
TANZBATT9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania walenga kuhamasisha amani DRC kupitia Kiswahili 

Kikundi cha tisa cha walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-9, kinachohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimeanza kusambaza daftari na vifaa vingine vya shule kwa watoto katika maeneo ya Mavivi huko BENI mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa lengo la kuwahimiza wanafunzi hao kuzungumza lugha ya Kiswahili ili wakimaliza shule waweze kuwasiliana na mataifa mengine.

Sauti
4'27"
TANZBATT 9

Lugha ya Kiswahili inatusaidia sana kwenye ulinzi wa amani DRC- Luteni Kanali Mley 

Lugha ya Kiswahili hivi sasa ni lugha ya kimataifa ikiwa imetengewa siku yake mahsusi ya kuadhimishwa ambayo ni tarehe 7 Julai kila mwaka. Wakati wa maadhimisho ya mwaka huu, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay alisema uamuzi wa Baraza Kuu la UNESCO kutambua lugha ya kiswahili kimataifa ulizingatia mambo kadhaa ya msingi ikiwemo nafasi ya lugha hiyo katika kusongesha amani.

Sauti
3'49"

22 JULAI 2022

Hii leo jaridani kubwa ni kutiwa saini huko Istanbul Uturuki kwa makubaliano baina ya Urusi, Ukraine na Umoja wa Mataifa ya kuwezesha nafaka na vyakula kutoka Ukraine viweze kusafirishwa kupitia Bahari Nyeusi. Shuhuda wa Umoja wa Mataifa kwenye utiaji huo saini si mwingine bali ni Katibu Mkuu mwenyewe wa UN, Antonio Guterres.

Sauti
12'59"
UN/Assumpta Massoi

Lugha ya Kiswahili imenipa ajira Umoja wa Mataifa

Kutana na Priscilla Lecomte, mtaalamu wa mawasiliano wa UN-CBi, mpango unaoratibiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP kushirikisha sekta binafsi katika kujiandaa kukabliana na majanga na hata kurejea katika hali nzuri baada ya majanga. Bi.

Sauti
2'31"

14 JULAI 2022

Jarida la leo lina Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Jifunze Kiswahili.

Katika Habari kwa Ufupi, Leah Mushi anamulika wito wa UNHCR wa kutaka sitisho la mapigano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako watu wanauawa na maelfu wanafurushwa. Kisha anamulika ripoti ya Umoja wa Mataifa kuwa ujira wa wanawake kwenye sekta ya afya ni wa chini kulinganisha na wanaume hata kama wako katika ngazi moja na mwisho ni wito kutoka UNCTAD wa kutaka bara la Afrika lisitegemee tu mazao na madini kupata fedha za kigeni bali iuze bidhaa za kihuduma.

Sauti
12'15"
Balozi Gertrude Mongella, akihojiwa na Stella VUzo wa UNIC Dar es salaam (Picha Maktaba)
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Acheni kutumia lugha msiyofahamu vyema, tumieni Kiswahili- Balozi Mongella

Miongoni mwa watu waliopokea kwa shauku kubwa kutambuliwa kwa lugha ya Kiswahili kimataifa ni aliyekuwa Rais wa Bunge la Afrika Balozi Gertrude Mongella kutoka Tanzania ambaye yeye amesema sasa anajivunia kujiita anatoka taifa linalozungumza lugha ya Kiswahili au Swahiliphone badala ya wale waingereza, Anglophone au wafaransa, Francophone.

Balozi Mongella amesema hayo katika mahojiano haya yafuatayo aliyofanya na Stella Vuzo wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC, jijini Dar es salaam nchini Tanzania wakati wa shamrashamra za kuelekea siku ya Kiswahili duniani tarehe 7 mwezi Julai mwaka huu.