Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kiswahili kuanza kutumika EAC rasmi mwaka 2024

Kiswahili kuanza kutumika EAC rasmi mwaka 2024

Pakua

Lengo namba 17 la Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs linataka uwepo wa Ushirikiano katika kufanikisha malengo. Ushirikiano huo unaweza kuwa baina ya nchi na nchi, wananchi na ushirikiano wa kikanda. Mwezi Desemba mwaka jana 2023 nilifunga safari hadi jijini Arusha nchini Tanzania na kuzungumza na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Peter Mathuki kutaka kufahamu namna wanavyoshirikiana na Umoja wa Mataifa katika maeneo mbalimbali ikiwemo ulinzi na usalama pamoja na kukuza lugha ya Kiswahili. Karibu usikilize mazungumzo yetu. 

Audio Credit
Leah Mushi/Dkt. Peter Mathuki
Sauti
7'40"
Photo Credit
UN News