Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

TANBAT 6, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wapokea pongezi kutoka JWTZ na MINUSCA

TANBAT 6, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wapokea pongezi kutoka JWTZ na MINUSCA

Pakua

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa Kikosi cha 6 cha kutoka Tanzania TANBAT 06 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) wamepokea ugeni na salamu kutoka Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia ujumbe uliongozwa na Brigedia Jenerali George Mwita Itang’are aliyewakilisha salamu za Mkuu wa Majeshi ya Tanzania kutokana na sifa nzuri anazozipokea kutoka MINUSCA kuhusu kikosi hicho. Afisa Habari wa TANBAT 06 Kapteni Mwijage Inyoma ameshiriki na kutuandalia makala hii..

Audio Credit
Selina Jerobon/Kapteni Mwijage Inyoma
Audio Duration
3'26"
Photo Credit
TANBAT 6/Kapteni Mwijage Inyoma