Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taasisi 16 zakutana Morogoro Tanzania kusongesha SDG 4

Taasisi 16 zakutana Morogoro Tanzania kusongesha SDG 4

Pakua

Taasisi 16 zikiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, asasi za kiraia na vyuo vikuu ambao kwa pamoja ni wanachama wa Mtandao wa Elimu Afrika Mashariki (RELI) wamekutana mjini Morogoro, Tanzania kujengewa uwezo wa namna ya kuimarisha juhudi za kuchochea mabadiliko ya elimu na kuhamasisha ujengaji fikra tunduizi kwa vijana ili kusongesha lengo namba 4 la Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu SDGs. Mafunzo haya yameratibiwa na Shirika lisilo la kiserikali la GESCI (The Global e-Schools and Communities Initiative) kutoka nchini Kenya linalotekeleza mradi wa ADAPT Kenya na Tanzania, Mwandishi wa Habari Hamad Rashid wa Redio washirika wetu MVIWATA FM ya Morogoro Tanzania amefuatilia mafunzo hayo ya siku tatu na kutuandalia makala ifuatayo.

Audio Credit
Selina Jerobon/Hamad Rashid
Audio Duration
5'10"
Photo Credit
Hamad Rashid