Mauritius waelekeza mbinu wanazotumia kutokomeza uvutaji wa tumbaku nchini mwao
Mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Afya WHO walitoa ripoti ya 9 kuhusu janga la uvutaji tumbaku na kueleza kuwa mafanikio yameanza kuonekana kwa nchi wanachama kutekeleza sera ya kulinda umma kutoathirika na uvutaji wa sigara unaofanywa na mtu mwingine ambapo zaidi ya watu bilioni 5.6 wamenufaika na sera hiyo ulimwenguni kote. Nchi ya Mauritius ilipongezwa kwa kuwa nchi pekee iliyotekeleza vyema sera zote sita za kupambana na athari za tumbaku. Je waliwezaje?