Wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja wataka kutambuliwa katika katiba mpya Tanzania
Umoja wa Mataifa, ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa na wanaharakati mbalimbali wa kupigania haki ikiwa ni pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali wameendelea kupaza sauti wakizitaka serikali duniani kutambua na kuheshimu haki za wanawake na wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja wanawake, au mashoga.