02 NOVEMBA 2022
Hii leo katika Habari za UN Assumpta Massoi anamulika masuala yafuatayo:
1. Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa hilo ikiwemo Kenya, Ethiopia na zaidi Somalia ambako maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako msitari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.