Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

08 Januari 2021

Leo ni Ijumaa na tunakuletea mada kwa kina na tunaangazia maonesho ya sanaa ya uchoraji picha yaliyofanywa jijini Nairobi Kenya na Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na madawa na uhalifu, UNODC. Picha hizo zimechorwa na watoto walioko chini ya uangalizi maalum wa kubadili tabia zao baada ya kukutwa na hatia za makosa mbalimbali nchini Kenya. Halikadhalika tunabisha hodi nchini Tanzania katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA kupata maana za maneno MCHAPO bila kusahau Habari kwa Ufupi ikimulika habari muhimu kwa siku ya leo. Mwenyeji wako ni Flora Nducha! karibu.

Sauti
11'29"

07 Januari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na wito wa Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres kwa mamlaka DRC kuchukua hatua kulinda raia na kuadhibu wahusika wa mauaji ya raia huko Beni, Kivu Kaskazini. Kisha anakwenda Ethiopia ambako watoto wa kiume wanashiriki kuepusha ndoa za utotoni za watoto wa kike. Bei za vyakula mwezi Desemba 2020 zimemulikwa na makala tunaangazia mchango wa WFP nchini Tanzania katika lishe bila kusahau mashinai tunamulika nafasi ya mboga za majani katika kuinua kipato cha vijana. Karibu!

Sauti
12'4"

06 JANUARI 2021

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa atoa wito wa kuhakikisha mizozo inasitishwa na mizizi yake kukatwa kwa lengo la kudumisha amani na kufikia ajenda ya maendeleo ya 2030 hususan brani Afrika.

-Walinda amani kutoka Burundi, Bangladesh na Cameroon waliopoteza maisha Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR wakati wa Krisimasi waagwa na kusafirishwa makwao kwa maziko

Sauti
11'34"

05 JANUARI 2021

Katika Jarida la Habari za UN hii leo Flora Nducha anakuletea

-Wakimbizi kutoka Tigray Ethiopia waendelea kumiminika Sudan na mahitaji yao yanaongezeka lasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR

-Kutana na Muhamiaji Mohammed Bushara ameye alienda Libya kusaka mustakbali bora lakini sasa amerejea nyumbani kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM na Muungano wa Ulaya Eu na kuanzisha biashara ya duka la vipodozi

Sauti
11'32"

04 JANUARI 2021

Katika Jarida la Habari za umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Watu zaidi ya 100 wauawa katika shambulio kwenye jimbo la Tillaberi nchini Niger, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani vikali shambulio hilo na kutaka wahusika wakamatwe na kuwajibishwa.

-Nchini Pakistan wachimba migodi ya makaa ya mawe 11 wameuawa katika shambulio la kigaidi lililotokea mwishoni mwa wiki kwenye jimbo la Balouchistan, watu wengine wengi wamejerihiwa na wengine kutekwa .

Sauti
10'6"