Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Waliojitokeza kushiriki uchaguzi wa CAR ni 75%- MINUSCA

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA umeripoti kuwa Mamlaka ya Kitaifa ya Uchaguzi ANE imetangaza baadhi ya matokeo ya uchaguzi siku ya Jumapili hii kulingana na kura zilizopigwa kwenye majimbo nane na asilimia 15 ya kura zilizopigwa nje ya nchi.

Hii ni kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric ambaye amewaambia leo waandishi wa habari mjini New York Marekani kwamba matokeo kamili yanatarajiwa kutolewa mwisho wa wiki hii na kuthibitishwa na Mahakama ya Kikatiba tarehe 15 Januari.

UN Photo/NICA

Ban amezungumza kwa simu na mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Saudia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amezungumza kwa njia ya simu na waziri wa mambo ya nje wa Saudia Abel bin Ahmed Al-Jubeir, na waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif.

Akizungumzana Bwana Zarif, Ban amerejea kauli yake kuhusu mauaji ya Sheikh al-Nimr na wafungwa wengine 46 yaliyotekelezwa na serikali ya Saudia Januari pili mwaka huu. Pia amezungumzia kulaani kwake vikali shambulizi dhidi ya ubalozi wa Saudia mjini Tehran na amemtaka waziri huyo wa mambo ye nje kuchukua hatua zinazohitajika kulinda maeneo ya kidplomasia nchini humo.

Somalia yaaga Nicholas Kay, aliyeitwa rafiki wa kweli

Aliyekuwa Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkuu wa Ujumbe wa Umoja huo nchini Somalia Nicholas Kay amehitimisha hivi karibuni muda wake kwenye nafasi yake.

Zaidi ya miaka miwili imepita tangu alipofika mjini Mogadishu mwezi Juni mwaka 2013 na viongozi wa Somalia pamoja na wafanyakazi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNSOM wameandaa hafla maalum kwa yule aliyetajwa kuwa rafiki wa ukweli wa Somalia.

Kwa mengi zaidi kuhusu hafla hiyo, ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.

Ethiopia yakumbwa na ukame mkali, WFP yatoa wito kwa ufadhili

Nchini Ethiopia, mahitaji ya kibinadamu yameongezeka mara tatu tangu mwanzo wa mwaka 2015 kutokana na ukame mkali unaokumba baadhi ya maeneo ya nchi.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP limesema El-Nino ambayo mwaka huu imekuwa mbaya zaidi imehatarisha zaidi hali hiyo na kusababisha mazao kuharibika, na mifugo kufa kwa wingi, huku utapiamlo wa kupindukia ukiathiri nusu ya wilaya za Ethiopia.

Ban Ki-moon alaani mauaji ya Sheikh Al-Nimr nchini Saudia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, ameeleza kushtushwa sana na mauaji ya watu 47 nchini Saudi Arabia, akiwemo Sheikh Nimr Baqir Al-Nimr, kama ilivyotangazwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Jumamosi hii.

Bwana Ban amesema hayo kwenye taarifa iliyotolewa na msemaji wake, akiongeza kwamba alikuwa amezungumzia kesi ya Sheikh Al-Nimr mara kadhaa na uongozi wa Saudia.

Sheikh An-Nimr na wafungwa wengine waliouawa tarehe pili Januari walihukumiwa kifo baada ya kesi iliyozua mashaka kuhusu usawa wake.

Martin Kobler atuma salamu za mwaka mpya kwa Walibya

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya Martin Kobler, ametuma salamu zake za mwaka mpya kwa raia wa Libya akiwatakia amani, matumaini na ukuaji wa uchumi.

Kwenye ujumbe wake uliotolewa tarehe mosi Januari, Bwana Kobler amesema ingawa mwaka wa 2015 haukuwa na baraka kwa Libya, makubaliano ya kisiasa yaliyosainiwa mwisho wa mwaka yameleta matumani, akiongeza kwamba mwaka 2016 utakuwa mwaka wenye fursa ya kukomesha mzozo wa Libya na kujenga upya amani na umoja wa nchi.

Ban Ki-moon apongeza Rais Museveni na Muungano wa Afrika kwa mazungumzo ya amani Burundi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha kuanzishwa upya kwa mazungumzo ya kisiasa baina ya pande kinzani za Burundi nchini Uganda.

Kwenye taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Katibu Mkuu amepongeza jitihada za Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye ni mpatanishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mazungumwo hayo.

Bwana Ban amezisihi pande za mzozo wa Burundi kushiriki kikamilifu kwenye mazungumzo hayo ili kukabili changamoto za kisiasa zinazoikumba nchi hiyo. Aidha amewaomba viongozi wa Burundi kuwajibika na kuipa kipaumbele amani na maridhiano.

Serikali zafikia makubaliano kuhusu mabadiliko ya tabianchi

Zaidi ya nchi 190 zimefikia makubaliano juu ya mazungumzo ya mabadiliko ya tabianchi.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya siku saba ya mazungumzo nchini Uswisi, katika utaratibu wa maandalizi ya kongamano kubwa litakalofanyika mjini Paris, Disemba mwaka huu.

Christiana Figueres, Katibu Mtendaji wa mkataba wa kimataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, ametangaza hayo alipozungumza na waandishi wa habari leo mjini Geneva.

Sauti
59"

Lugha ya Kiswahili yazidi kuenea kwenye medani za kimataifa

Kwa mara ya kwanza ripoti ya Maendeleo ya binadamu inayoandaliaw na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa imekuwa na muhtasari wake katika lugha ya Kiswahili. Uzinduzi wa muhtasari huo ulifanyika Kilifi, Mombasa Kenya tarehe 12 mwezi huu wa Juni na siku ya Alhamisi ya tarehe 20 Juni mjini New York Marekani, ubalozi wa Kenya ukafanya uwasilishaji wa muhtasari huo. Je nini kilijiri? Ungana na Assumpta Massoi katika makala hii ya wiki.

STUDIO: ASSUMPTA pckg