Ban aipongeza Sri Lanka kwa mwaka mmoja wa kipindi cha mpito
Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon amempongeza Rais wa Sri Lanka, Maithripala Sirisena, serikali na watu wa nchi hiyo kwa kutimiza mwaka mmoja wa serikali ya mpito wa kisiasa.
Ban ametiwa moyo na serikali kujidhatiti katika ajenda ya mabadiliko ambayo yana lengo la kuhakikisha amani ya kudumu , utulivu na mafanikio kwa watu wa Sri Lanka.
Katibu mkuu anatambua hatua za awali zilizochukuliwa na serikali kuimarisha utawala bora, hatua za awali za maridhiano na utekelezaji azimio la baraza la haki za binadamu la Oktoba 2015.