Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Sigrid Kaag akutana na waziri mkuu wa Lebanon

Mratibu maalumu wa Umoja wa mataifa kwa ajili ya Lebanon Bi Sigrid Kaag leo Alhamisi amekutana na waziri mkuu wa Lebanon Tammam Salam aliporejea kutoka Saudi Arabia kwenye  ziara ya kikazi.

Bi Kaag amempa taarifa waziri mkuu huyo kuhusu mkutano wake na waziri wa mambo ya nje wa Saudia Adel Al-Jubeir na maafisa wengine wa serikali. Majadiliano yake na viongozi wa Saudia yalijikita kwenye masuala ya siasa, usalama na urejeshaji wa utulivu Lebanon na katika kanda nzima.

Mkuu wa UM nchini CAR azungumza na wagombea urais

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR Parfait Onanga-Anyanga amekutana leo na wagombea urais 28 miongoni mwa 30 waliogombea katika uchaguzi uliofanyika tarehe 30, Disemba, mwaka 2015.

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric aliyezungumza na waandishi wa habari leo mjini New York Marekani akisema kwamba bwana Onanga-Anyanga amesisitiza umuhimu wa kuendeleza mchakato wa uchaguzi.

Naondoka Mali nikiwa na matumaini; Hamdi

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Mali, Mongi Hamdi amesema anaondoka Mali na moyo wa amani na uaminifu kuhusu mchakato wa amani.

Amesema hayo kwenye ujumbe wake wa mwisho akihitimisha muda wake kama mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Mali MINUSMA, akimshukuru Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keita, wawakilishi wa serikali na jamii wa Mali kwa ushirikiano wao na MINUSMA katika kujenga amani ya kudumu nchini humo.

Baraza la Usalama laahidi hatua kali kufuatia madai ya jaribio la nyuklia DPRK

Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wamelaani vikali jaribio la nyuklia lililofanywa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea, DPRK, leo Jumatano ya Januari 6, kufuatia kikao kikao cha dharura walichokuwa nacho leo kushughulikia suala hilo nyeti.

Taarifa ya Baraza la Usalama ilotolewa na Msemaji wa Katibu Mkuu imesema kuwa jaribio hilo la DPRK ni ukiukwaji dhahiri wa maazimio ya Baraza hilo namba 1718 (2006), 1874 (2009), 2087 (2013), na 2094 (2013) na kanuni ya kutoeneza silaha za nyuklia, na hivyo ni tishio bayana kwa amani na usalama wa kimataifa.

CTBTO yaendelea kuchambua taarifa za jaribio la mlipuko DRPK

Wataalamu wa Shirika la Mkataba wa Kupiga Marufuku Majaribio ya silaha za Nyuklia, CTBTO, wanaendelea na kazi ya kutathmini ripoti za mitetemo iliyobainika kwenye eneo la Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Korea, DPRK.

Katibu Mtendaji wa CTBTO Lassina Zerbo amesema hayo akihojiwa na Radio ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya simu kutoka Ouagadougou akieleza kuwa vituo akihojiwa na Radio ya Umoja wa Mataifa amesema..

(Sauti ya Lassina)

MENUB.

Burundi yakataa mazungumzo ya kisiasa, UM waiomba ishiriki

Umoja wa Mataifa unaiomba serikali ya Burundi ishiriki mazungumzo ya kisiasa, ukielezea kuendelea kuwa na wasiwasi kuhusu mauaji yanayozidi nchini humo.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric amesema hayo akijibu swali wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo mjini New York Marekani alipoulizwa msimamo wa Umoja huo kuhusu tangazo la Burundi la kukataa kushiriki mazungumzo ya amani huko Arusha, Tanzania.

(Sauti ya Bwana Dujarric)

Malawi ni kinara wa mapitio ya upunguzaji wa hatari za majanga Afrika:UNISDR

Afrika imefungua ukurasa mpya katika harakati zake za utekelezaji wa mkataba wa Sendai kwa ajili ya kupunguza hatari ya majanga. Kinara ni Malawi, ambayo imefanyia tathimini na kuzipitia sera na hatua zake takribani mwaka mmoja baada ya kukumbwa na mafuriko makubwa.

Tathimini ya siku kumi nchini Malawi iliyofanywa na wataalamu watatu kutoka Msumbiji, Afrika Kusini na Zimbabwe mwezi Disemba imezindua mchakato ambao utakamilisha katika miezi ijayo uwasilishaji wa ripoti ya kwanza kabisa barani Afrika ya mapitio rika kuhusu upunguzaji wa hatari ya majanga.