Malawi ni kinara wa mapitio ya upunguzaji wa hatari za majanga Afrika:UNISDR
Afrika imefungua ukurasa mpya katika harakati zake za utekelezaji wa mkataba wa Sendai kwa ajili ya kupunguza hatari ya majanga. Kinara ni Malawi, ambayo imefanyia tathimini na kuzipitia sera na hatua zake takribani mwaka mmoja baada ya kukumbwa na mafuriko makubwa.
Tathimini ya siku kumi nchini Malawi iliyofanywa na wataalamu watatu kutoka Msumbiji, Afrika Kusini na Zimbabwe mwezi Disemba imezindua mchakato ambao utakamilisha katika miezi ijayo uwasilishaji wa ripoti ya kwanza kabisa barani Afrika ya mapitio rika kuhusu upunguzaji wa hatari ya majanga.