UNAMID yahimiza utulivu kufuatia hali tete Darfur Magharibi
Ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika Darfur, UNAMID, umeeleza kutiwa hofu na hali tete inayoendelea katika mji wa El Geneina na karibu na kijiji cha Mouli, yapata kilomita 15 kutoka El Geneina, Darfur Magharibi. Kwa mantiki hiyo, UNAMID imetoa kwa mamlaka za serikali kufanya juhudi zote kuidhibiti hali.
Taarifa ya UNAMID imesema kuwa hali hiyo tete imeibuka kufuatia kikundi kisichojulikana kukivamia kijiji cha Mouli mnamo Januari 9 2016, na kusababisha idadi kubwa ya wanakijiji hicho kukimbilia El Geneina.