Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

© UNICEF/Karin Schermbrucker

WHO Zambia yashirikiana na Serikali kutokomeza Kipindupindu

Juhudi na ushirikiano wa pamoja wa wahudumu wa afya, vituo na Jamii, vimefanikisha kukomesha mlipuko wa kipindupindu uliozuka nchini Zambia kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO nchini Zambia, ambalo limeeleza kwamba ugunduzi wa mapema na matibabu husaidia kukabiliana na ugonjwa huo na kupunguza idadi ya vifo. 

Jioni moja Philta Samazimva alilalamika ghafla tumbo kuuma, baada ya kuharisha sana, mama yake mzazi Hildar Samazimba alimpeleka kliniki.

Sauti
2'9"
Shpend Bërbatovci

Guterres: Tekelezeni kikamilifu mkataba wa mwaka 1994 wa kuwalinda wafanyakazi wa UN

Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu kuenzi ujasiri na kujitolea kwa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu kila mahali kokote waliko kwa kuahidi kuwalinda na kuwaunga mkono wanaposaidia kujenga dunia yenye amani zaidi na ya utu kwa ajili ya watu wote. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Sauti
1'45"
UNEP/Lisa Murray

Umoja wa Mataifa yataka nchi kuwa na makubaliano ya ushirikiano wa matumizi ya vyanzo vya maji

Leo ni siku ya maji duniani chini ya kauli mbiu Maji kwa amani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa siku hii amehimiza nchi kuhakikisha zinashirikiana na kuwa na makubaliano ya kutumia vyanzo vya maji. 

Katika ujumbe wake huo Guterres ameeleza kuwa mpaka sasa ulimwenguni “Nchi 153 zinashirikiana vyanzo vya maji lakini ni nchi 24 pekee zenye makubaliano kwa vyanzo vyao vyote vya maji wanavyoshirikiana.” 

Sauti
1'57"
© WHO

WHO: Madaktari Gaza wanafanyakazi kutwa kucha kuokoa maisha bila kutia chochote tumboni

Wahudumu wa afya Gaza wanafanya kazi mchana kutwa na usiku kucha wakihaha kuokoa Maisha ya wagonjwa na majeruhi katika hospitali chache zilizosalia zikifanyakazi bila kutia chochote tumboni kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO. 

WHO inasema wafanyakazi hao wanaolazimika kufanyakazi saa 24 kuokoa maisha ya watu kama ambavyo wanakosa vifaa muhimu na vitendeakazi vingine vivyo hivyo wanakosa chakula cha kutosha kama ilivyo kwa maelfu mengine ya raia wa Gaza.

Sauti
2'32"
UNICEF Yemen

UNICEF yatumia watoto kuhamasisha jamii kupata chanjo nchini Yemen

Katika kuhakikisha watoto wanapata chanjo zote zinazohitajika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Yemen limekuja na mbinu ya kutumia watoto kuhamasisha jamii kupeleka watoto kupata chanjo. 

Mtoto Leen mwenye umri wa miaka 10 kutoka nchini Yemen, anasema kupitia mpango wa ufadhili wa mtoto, programu inayotumia watoto kwenda kuhamasisha jamii kupata chanjo ili wawe na afya bora amefanikisha watoto 150 kupata chanjo katika jamii yake.  

Sauti
2'6"
© UNRWA

FAO: Baa la njaa lanyemelea Gaza

Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya  hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani. 

Sauti
2'7"