Muda wa maneno umekwisha tuchukue hatua tuokoe wanawake- Bi. Mohammed
Baada ya ziara yao kwenye nchi za Sudan Kusini, Chad na Niger, viongozi wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden, leo wamewasilisha ripoti zao mbele ya wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wa kikao kuhusu wanawake, amani na usalama barani humo.