Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Viongozi Sudan Kusini pigeni moyo konde- UN

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed akimkumbatia msichana mdogo wakati wa ziara ya Sudan Kusini
UN Photo/Isaac Billy
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed akimkumbatia msichana mdogo wakati wa ziara ya Sudan Kusini

Viongozi Sudan Kusini pigeni moyo konde- UN

Amani na Usalama

Hatutachoka kutafuta amani ya kudumu  katika taifa la Sudan Kusini, amesema Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J.Mohammed wakati wa ziara yake aliyoanza leo nchini humo yenye lengo la kukuza umuhimu wa wanawake katika kuzuia migogoro.

Amesema ni kwa muktadha huo amekwenda nchini humo ambapo pia lengo ni

(Amina J. Mohammed)

 “Kuwaambia nilichosikia viongozi wa Afrika wakisema, ni kuwa sasa viongozi nchini Sudan Kusini  sharti wapige moyo konde na wabadilike pamoja na kuwajibika kuhusu amani ya nchi yao.”

 

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed amekwenda na ujumbe wa matumaini na amani nxchini Sudan Kusini
UN Photo/Isaac Billy
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed amekwenda na ujumbe wa matumaini na amani nxchini Sudan Kusini

 

 Kuhusu unyanyasaji wa kingono katika migogoro, Naibu Katibu Mkuu amesema kuwa Umoja wa Mataifa unajaribu kadri ya uwezo wake kulishughulikia suala hilo.

(Amina J. Mohammed)

 “ Hapa tuna mshauri maalum wa dhuluma za kingono dhidi ya wanawake katika sehemu za migogoro ya kivita ili kuweza kuwasilisha malalamiko yenu kwa jamii ya kimataifa na  hivyo tuwezeshe viongozi kufanya mambo mazuri.”

Katika ziara hiyo, Bi. Mohammed anaandamana na mjumbe maalum wa Muungano wa Afrika  anayehusika na  masuala ya wanawake, amani na usalama Bineta  Diop.

Akiwa nchini humo Naibu Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa anakutana na makundi mbalimbali pamoja na ya viongozi wa wanawake, kidini na wa makundi ya kiraia.