Matumaini ya kupitishwa azimio na Baraza la Usalama juu ya Lebanon na Israel
TMY:Kama tulivyo kuelezeni hapo awali katika ripoti zetu za leo tuna anza na hali ya huko Lebanon.
TMY:Kama tulivyo kuelezeni hapo awali katika ripoti zetu za leo tuna anza na hali ya huko Lebanon.
TMY:Matokeo mengine muhimu kwa wiki hii ni hali baada ya uchaguzi wa kihistoria ya huko jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
Likiwapongeza wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kushiriki katika uchaguzi wa kihistoria wa nchi yao, kwa sehemu kubwa kabisa kwa amani, siku ya Jumapili, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitoa mwito wiki hii kuwataka wawe watulivu na kusubiri matokeo ya mwisho ya uchaguzi.
Mjumbe maalum wa UM huko Somalia, Francois Lonseny Fall, amepongeza tangazo la sera lililotolewa na mawaziri wa nchi za mamlaka ya maendeleo ya pembe na Afrika ya mashariki IGAD, likidai kufuata sera za UM huko Somalia.
Afisi ya kulinda amani ya UM huko Burundi ONUB imeeleza kushangazwa na ripoti kua kulikuwepo na jaribio la kuipindua serekali ya Bujumbura, siku chache zilizopita na kwamba kuna wanasiasa mashuhuri walotiwa vizuizini.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto UNICEF limelaani vikali sana habari za kutokea vitendo zaidi vya ubakaji huko Zimbabwe na likihimiza sheria mpya kupitishwa kuwalinda watoto wa nchi hiyo na kutoa masomo zaidi juu ya virusi vua HIV na Ukimwi.
wiki hii jumuiya ya kimataifa imeisifu serekali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo kwa kufanikiwa kutayarisha na kufanya uchaguzi wa kwanza kabisa wa vyama vingi katika kipindi cha zaidi ya miaka 40 iliyopita.
Shirika la UM juu ya Operesheni za Amani katika Sudan, UNMIS, limeripoti karibuni ya kuwa wafanyakazi wa kimataifa wanaosimamia huduma za kiutu katika Darfur wanakabiliwa na vizingiti vinavyokwamisha huduma za kuwasaidia raia kupata mahitaji ya kunusuru maisha kwa sababu ya kuendelea kwa mashambulio na hali ya utumiaji nguvu dhidi yao, pamoja na vitendo vya uharamia na mapigano yalioshtadi kati ya makundi ya waasi.~~
Naibu KM wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Amani Duniani, Jane Holl Lute aliripoti mbele ya Baraza la Usalama wiki hii kwamba wanajeshi waangalizi wanne wa ulinzi wa amani wasiochukua silaha kutoka Austria, Kanada, Finland ~na Uchina, waliuawa Ijumanne kwa mizinga ya majeshi ya Israel ambayo tuliarifiwa ililengwa moja kwa moja, sawia, kwenye kituo cha uangalizi cha UM karibu na mji wa Khiam, Lebanon ya kusini.
Ilivyokuwa matatizo ya kiutu bado yanaendelea kukithiri katika mazingira ya vita katika Lebanon ya kusini UM umeripoti ya kuwa utalazimika kupeleka misafara ziada ya misaada ya kihali katika miji ya Jezzine na Sidon ili kukidhia mahitaji ya kunusuru maisha kwa umma waathiriwa wa maeneo haya. Hatua hii imechukuliwa baada ya msafara wa UM kufanikiwa Ijumanne kupeleka katika mji wa bandari wa Tyre shehena za chakula na mahitaji mengineyo ya kiutu.