Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya usalama katika Darfur yazidi kuharibika

Hali ya usalama katika Darfur yazidi kuharibika

Shirika la UM juu ya Huduma za Amani katika Sudan (UNMIS) limeripoti kuwa hali ya usalama katika Darfur ya kusini, inaendelea kuharibika, hususan katika mji wa Gereida, kutokana na mvutano uliojiri na uhasama kati ya makabila yanoishi kwenye eneo hilo. Wakati huo huo kwenye mji wa Um al-Kher, Darfur ya Magharibi imeripotiwa kutukia vifo vya watu walioambukizwa na maradhi ya kipindupindu. Ripoti ya karibuni ya KM imeonya ya kuwayale mashirika yanayohudumia misaada ya kiutu huenda yakafunga operesheni zake pindi hali ya usalama haijadhibitiwa katika eneo kama ipasavyo. ~~

Kwa taarifa kamili sikiliza idhaa ya mtandao.