Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tabaka la hewa kingifu la ozone katika Antartica limeharibiwa kima kikubwa katika 2006

Tabaka la hewa kingifu la ozone katika Antartica limeharibiwa kima kikubwa katika 2006

Shirika la UM juu ya Vipimo vya Hali ya Hewa (WMO) limeripoti ya kwamba tabaka la hewa kingifu la ozone katika eneo la ncha ya kusini ya dunia la Antartica, limethibitika kuharibiwa kwa kima kikubwa kabisa mno mwaka huu. Uharibifu huu husababisha miale ya jua kupenya kwa wingi zaidi kwenye mazingira ya kimataifa, na hukithirisha maradhi ya sartani kwa umma wa ulimwengu.