Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Takwimu ziada juu ya Zimbabwe na kipindupindu

Takwimu mpya kuhusu mripuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika Zimbabwe, zilizosajiliwa na kuthibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) mnamo tarehe 25 Disemba zinaonyesha idadi ya wagonjwa wa maradhi hayo siku hiyo ilikuwa 26,497, wakati jumla ya vifo vilirikodiwa ilifikia 1,518.~

Hapa na Pale

WHO imeripoti hivi sasa wataalamu wa idara zinazohusika na matibabu ya magonjwa ya miripuko, wamejumuika na Wizara ya Afya na washiriki wengine wa kimataifa, kuratibu miradi maalumu itakayoongozwa na Kituo cha Udhibiti wa Kipindupindu, kwa madhumuni ya kuhudumia bora sekta ya afya ili kukomesha, halan, uenezaji wa maradhi nchini. Kwa mujibu wa taarifa ya WHO sekta ya

Hapa na Pale

Shirika la UM Kulinda Amani katika JKK (MONUC) limearifu Ofisi juu ya Ukaguzi wa Makosa ya Kikazi (OIOS) inaendeleza uchunguzi kuhusu tuhuma za kuwa baadhi ya wahudumia amani katika eneo la Kivu Kaskazini walishiriki kwenye vitendo vibaya dhidi ya raia. MONUC insasema baadhi ya vitendo hivyo hujumuisha ukandamizaji na udhalilishaji wa kijinsiya. MONUC iliongeza kusema kwa kuhadharisha ya kwamba hadi sasa hivi tuhumu hizo ni madai ambayo bado hayajathibitishwa kisheria. Watumishi wote wa MONUC wamenasihiwa kushirikiana kikamilifu na wachunguzi wa Ofisi ya OIOS.