Kampeni ya mshikamano na wakimbizi yang’oa nanga
Siku ya kimataifa ya michezo kwa maendeleo na amani yaangaziwa huku kampeni maalum ikizinduliwa.
Siku ya kimataifa ya michezo kwa maendeleo na amani yaangaziwa huku kampeni maalum ikizinduliwa.
Kama mliweza kuungana na kupitisha azimio kudhibiti silaha za kemikali nchini Syria, sasa mwashindwa nini kuendelea na umoja huo hadi silaha hizo zitokomezwe? Ahoji Markram.
Syria! Syria! Syria! Bado ni kizungumkuzi, maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanapitishwa lakini wahusika ni kama kusema "wameweka pamba masikioni."
Choo kimoja kutumiwa na watu 200, gharama ya yai moja ni dola 4, mfuko mmoja wa mkate dola 4, ni simulizi kutoka kwa wakimbizi walioweza kukimbia kutoka eneo la Ghouta Mashariki nchini Syria.
Mwaka wa 7 wa mzozo wa Syria umekamilika na sasa mwaka wa 8 umeanza na hakuna nuru ya kumalizika kwa mzozo huo, lakini bado tusikate tamaa, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo.
Hatimaye misaada ya kibinadamu imewasili Ghouta Mashariki kiunga cha mji mkuu wa Syria, Damascus ikiwa ni ya kwanza tangu katikati ya mwezi Februari.
Kamisha mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo ametoa wito wa mgogoro wa Syria kufikishwa kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC.
Mapigano makali yameendelea leo asubuhi kwenye eneo la Ghouta Mashariki nchini Syria licha ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kutaka sitisho la mapigano kwa siku 30 ili misaada ifikie wahitaji na wagonjwa waweze kuhamishwa.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio namba 2401 la usitishwaji wa mapigano kwa siku 30 katika eneo la Ghouta mashariki nchini Syria na mji mkuu Damascas, ili kupisha misaada ya kibinadamu.
Syria hali inazidi kuwa mbaya zaidi , raia wanakabiliwa na mashambulizi. Tangu tarehe 4 mwezi huu wa Februari raia zaidi ya 300 wameuawa kwenye mapigano kati ya serikali na wapinzani.