Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Baada ya kuporwa utoto wao na vita, sasa maelfu ya watoto waishia ukimbizini Uganda

Wahudumu wa mashirika ya misaada ya kibinadamu nchini Uganda wakiwemo wa Umoja wa Mataifa wanakumbana na changamoto kubwa ya kuwasaidia watoto wakimbizi zaidi ya 25,000 waliotengana na wazazi ama walezi wao kutokana na vita na kusaka hifadhi wakiwa peke yao nchini humo. Mwandishi wetu wa Uganda  John Kibego ametembelea makazi ya wakimbizi ya Imvepi Wialayani Arua nchini humo ambako kuna asilimia kubwa ya watoto  na kuandaa tarifa hii.