Ukata walazimu WFP kusitisha mgao wa chakula kwa watu 100,000 Sudan Kusini
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP limesema litasitisha kwa miezi mitatu mgao wa msaada wa chakula kwa zaidi ya wakimbizi wa ndani 100,000 nchini Sudan Kusini kuanzia mwezi ujao wa Oktoba kutokana na ukata.