Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko

Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko

Pakua

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unaendelea katika huko Glosgow na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa amewaeleza viongozi wa ulimwengu kuwa ni muhimu kuchukua hatua sasa kwani wanadamu wanajichimbia kaburi, nchini Uganda jamii ya Watyaba, mojawapo ya jamii za walio wachache wanaoishi katika viunga vya Ziwa Albert, wanapaza sauti kwa serikali na shirIka  la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwasaidia kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa takwimu za serikali ya uganda, tzaidi ya watu  300,000 wameathiriwa na  mafuriko kote nchini Uganda.

Basi ungana na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego ili kufahamu hali halisi katika mahojiano baina yake na Badru Kantanda, kiongozi wa Watyaba.

Audio Credit
John Kibego
Audio Duration
3'45"
Photo Credit
UN/ John Kibego