Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN/ John Kibego

Wakimbizi wakaribisha juhudi za UN Women kuwezesha wanawake, Uganda

Nchini Uganda jamii ya wakimbizi katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wamekaribisha mradi wa kuwawezesha na kushughulikia mizozo katika jamii hiyo unaotekelezwana shirika la National Association oF Professional Environmentalists (NAPE), kwa msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake, UN-Womnen. Mwandishi wetu John Kibego amezungumza na walengwa wa mradi huo wa miaka miwili ambao pia utawanufaisha wenyeji walioko katika makazi ya wakimbizi wa ndani ya Rwamutonga na Kigyayo. Je, wakimbizi wenyewe wanataka ujikite katika masuala gani?

Sauti
3'40"
UN SDGs

Raia wa Uganda wahimiza bunge jipya kuzingatia utekelezaji wa SDGs

Serikali kote dunani zina mchango mkubwa katika utekelezaji wa malenngo ya maendeleo endelevu au SDGs. Nchini Uganda viongozi wa ngazi mbalimbali wa kisiasa wameapishwa  baada ya kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwanzoni mwa mwaka huu. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amevinjari kusaka yale ambayo raia wa Uganda  wanatarajia wabunge hao kufanya ili malengo ya maendeelo endelevu yafikiwe katika muongo huu wa mwisho kuelekea mwaka 2030. Ungana naye katika makala ifuatayo.

Sauti
3'31"
UN/ Jason Nyakundi

Ndugu watatu wa kiume wajikimu kwa kazi ya ufundi nchini Uganda

Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 61 ya watu walioajiriwa duniani, wanapata kipato chao kupitia ajira katika sekta isiyo rasmi. Kwa bara la Afrika, asilimia 85.8 ya ajira zote ni katika sekta hiyo isiyo rasmi ambapo Umoja wa Mataifa unasema idadi kubwa ya waajiriwa huko ni wanaume.

Sauti
3'55"
UN/UNIC Nairobi

Nilipokea taarifa za ushindi nikwa nyumbani na kwa kweli nilijawa nafuraha sana-Meja Nyaboga

Chanda chema huvikwa pete walinena wahenga na hali ni kama hiyo kwa mlinda amani kutoka Kenya ambaye amechaguliwa kupokea tuzo ya Umoja wa Mataifa ya mwanajeshi mwanaharakati wa masuala ya kijinsia kwa mwaka 2020.  

Meja Steplyne Nyaboga ambaye alikuwa mshauri wa kijeshi wa masuala ya kijinsia alipohudumu katika operesheni ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika wa kulinda amani Darfur (UNAMID) katika mahojiano maalum na Grace Kaneiya akiwa huko Nairobi Kenya amesema alipokea habari za ushindi, “kwa furaha isiyo kifani” 

Sauti
3'43"
UNFPA/Luis Tato

UNFPA na Taasisi ya Panzi DRC yaingia makubaliano kunusuru manusura wa ukatili wa kingono 

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yamekuwa mwiba siyo tu katika usalama wa taifa hilo bali pia kwa wanawake na wasichana ambao hukumbwa na ukatili wa kingono kule kwenye mapigano. Mashirika ya kiraia yamekuwa yakiunga mkono harakati za Umoja wa Mataifa za kuhakikisha manusura wa ukatili huo wanarejeshewa siyo tu utu lakini pia kujiamini na kuendelea na maisha. Miongoni mwa mashirika hayo ni taasisi ya hospitali ya Panzi inayoongozwa na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Dokta Denis Mukwege.

Sauti
4'57"
Delight Uganda Limited

Tuzo ya UNCTAD imenipa motisha zaidi kusaidia jamii – Dkt Julian Omalla

Mshindi wa tuzo ya wanawake wajasiriamali iliyotolewa na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD na pia akapigwa jeki ya mkopo nafuu wa dola milioni 10 kutoka kwa serikali ya Uganda ameeleza alivyopokea tuzo hiyo na mipango ya baadaye. Akizungumza na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego, Dkt Julian Omalla ambaye amejipatia umaarufu kutokana na shughuli za kujikwamua pamoja na maelfu ya wanawake na vijana, amesema amepata maono makubwa zaidi baada ya kutunikiwa tuzo.

Sauti
3'42"
Pete Muller for the ICC

Mradi wa UN Women wa haki za ardhi za wanawake wakaribishwa, Uganda

Mradi wa UN Women wa kuimarisha ulinzi wa haki za ardhi za wanawake umeleta matumaini makubwa ya kupiga jeki juhudi za serikali kupambana na vikwazo vya kimila vinavyowakera wanawake nchini Uganda.

Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego baada ya kuzungumza na wadau kadhaa wa masuala ya jinsia na maendeleo kuhusu mradi huo unaotekelezwa na shirika la kiraia la Mid-western Anti-corruption Coalition, MIRAC, ametuandalia makala ifuatayo.

Sauti
3'33"